Tuesday, August 13, 2013

Juliani: the illest Kenyan Hip Hop Mc...

Jina la Juliani ni geni sana masikioni kwa watu wengi ambao hawafuatilii muziki kiundani, lakini kwa wale wenye mapenzi ya kweli na muziki na wanaosupport mziki wa kweli, Juliani si jina geni kwao, na ni mmoja kati ya wanaharakati na wana Hip Hop mahiri waliosalia nchini Kenya, Africa na Duniani kwa ujumla.




Jina la juliani, na nyota yake ilianza kung'aa pale alipotoka na "bahasha ya Okampo"  akitoa hisia zake hali ilivyo nchini Kenya kuhusu masuala ya uongozi na siasa kiujumla, haki na uhuru wa raia wa Kenya.

Kama umepata kusikia na kuyafuatilia mashairi yake, Juliani huongelea sana mambo ya siasa hasa za Kenya, akitoa taswira na picha halisi kuhusu vuongozi na maovu yanayofanywa na viongozi hao.
Kwa upande wake yeye anaiongelea kenya, lakini katika hali halisi, haya ni matatizo ya waafrika na hasa tanzania ambayo yanatukabili.

Hip Hop ni kuongelea ukweli wa  mambo na matatizo ya jamii tunazoishi na kutuzunguka, na hili linanifanya nipende sana kumsikiliza juliani kwa sababu anasimamia ukweli huo na nguzo.



Kibao Chake "Utawala" ni wimbo unaosisimua na kuvuta hisia, kwani ameongelea ukweli na hali halisi ya viongozi, uongozi wetu, makosa tunayofanya sisi na yale yanayofanywa na viongozi wasio na weledi(wanasiasa feki).



"niko njaa hata siwezi karanga, 
  hohe haaaheee, shaghalabaghala,
  niko tayari, kulipa gharaama,
  sitosimama maovu yakitawala..."
hayo ni baadhi ya maneno yanayopatikana katika wimbo huo "Utawala".

usikilize hapa..




No comments:

Post a Comment

type in here..